Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CR7 asitisha mgomo wake, akubali kurejea uwanjani Al Nassr

Ripoti mbalimbali kutoka vyanzo vya kuaminika nchini Saudi Arabia zinaeleza kuwa nyota wa kimataifa Cristiano Ronaldo, amesitisha rasmi mgomo wake na yuko tayari kurejea uwanjani kuitumikia klabu ya Al Nassr, baada ya wafanyakazi wote wa klabu hiyo kulipwa mishahara na posho zao walizokuwa wanadai.

Hatua hiyo inakuja baada ya mvutano uliodumu kwa muda kati ya Ronaldo na Tume ya Uwekezaji ya Saudi Arabia, inayofahamika kama Saudi Public Investment Fund (PIF).

Inadaiwa kuwa nahodha huyo wa timu ya taifa ya Ureno alikuwa na malalamiko makubwa kuhusu kile alichodai kuwa ni upendeleo unaotolewa kwa baadhi ya klabu, hususan katika masuala ya usajili wa wachezaji na uwekezaji, jambo ambalo aliona linaathiri ushindani wa haki ndani ya ligi.

Mbali na kulalamikia mwenendo wa usajili ambao haukuwa na tija kwa Al Nassr, Ronaldo pia alichukua msimamo mkali wa kugoma kushiriki mazoezini na mechi ili kushinikiza haki za wafanyakazi wa klabu hiyo, hasa wale wa ngazi za chini, ambao kwa muda walikuwa hawajalipwa stahiki zao.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Ronaldo alisisitiza kuwa heshima na ustawi wa wafanyakazi ni msingi muhimu wa mafanikio ya klabu yoyote.

Baada ya madai hayo kushughulikiwa na malipo kufanyika kwa wafanyakazi wote, Ronaldo ameridhia kurejea kikosini na kuendelea na majukumu yake ya kuiongoza Al Nassr uwanjani.

Kurejea kwake kunatarajiwa kuipa nguvu mpya timu hiyo katika michezo ijayo, huku mashabiki wakitarajia kuona nahodha wao akirejea katika kiwango chake cha juu na kuisaidia klabu kupigania malengo yake ndani na nje ya Saudi Arabia.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa