Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mashabiki Simba wanataka Aucho asajiliwe

Mara baada ya klabu ya Simba Sc kufanikiwa kuinasa saini ya aliyekua kiungo mshambuliaji wa klabu ya Singida Black Stars Clatous Chota Chama, mashabiki wa klabu ya Simba Sc wameonyesha wazi matamanio yao ya kutaka kuona viongozi wao wanafanya jitihada za kuinasa saini ya kiungo mkabaji wa klabu hiyo raia wa Uganda anayejulikana kwa majina ya Khalid Aucho.

Khalid Aucho ni moja kati ya mastaa wa klabu ya Singida Black Stars ambao wamempongeza Chama kujiunga na klabu ya Simba Sc na salamu zake za pongezi amezichapisha kwenye ukurasa rasmi wa Instagram unaotumiwa na Clatous Chota Chama.

Mara baada ya Aucho kumpongeza Chama kwa kusajiliwa na klabu ya Simba Sc, mashabiki wa klabu ya Simba Sc wametimia nafasi hiyo kumuomba Aucho aungane na Chama kwenye kikosi chao ambacho kinaonyesha kuwa na madhaifu mengi msimu huu haswa kwenye eneo la kiungo.

Mashabiki hao wameonyesha kuvutiwa zaidi na ubora wa Khalid Aucho na wanaamini kwamba huyu ni mchezaji wa daraja la juu sana ambaye kama atasajiliwa na viongozi wa klabu yao basi anaweza kuongeza kitu kikubwa sana kwenye eneo lao la kiungo.

Khalid Aucho hajataka kupepesa macho kwenye sakata hili bali ameibuka na kujibu maombi ya mashabiki wa klabu ya Simba Sc kwa kuweka emoji za kucheka akiwa na maana kwamba amefurahishwa na kile ambacho mashabiki hao wamekifanya.

Khalid Aucho mpaka sasa bado ni mchezaji halali wa klabu ya Singida Black Stars lakini Simba Sc bado wanayo nafasi ya kupambana zaidi kama watakuwa wanahitaji saini yake haswa katika dirisha hili la usajili kwani nyota huyo hana changamoto ya kuchagua timu ya kuitumikia bali anaangalia maslahi.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa