Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Makonda atanii, akutana na Rais wa FIFA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mheshimiwa Paul Makonda amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Shirikisho la Kandanda Duniani (FIFA) Bw. Gianni Infantino katika ofisi za FIFA zilizopo Jijini Rabat, nchini Morocco.

Katika mazungumzo hayo Mheshimiwa Makonda amemshukuru Bw. Infantino kwa ushirikiano mkubwa anaoutoa kwa Tanzania katika maendeleo ya mchezo wa mpira wa miguu na amemhakikishia kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali anayoiongoza inaunga mkono jitihada hizo na ipo tayari kushirikiana na FIFA.

Mheshimiwa Makonda amemueleza Bw. Infantino kuwa Tanzania inazo fursa nyingi za kuchangia katika maendeleo ya mpira wa miguu vikiwemo vipaji vya vijana wengi, maeneo ya kujenga miundombinu ya michezo na utashi wa kisiasa, na kwamba FIFA inakaribishwa kushirikiana na Serikali katika uwekezaji huo.

Aidha, Mheshimiwa Makonda amemkaribisha Tanzania Bw. Infantino na amemwambia Tanzania ipo tayari kuwa mwenyeji wa matukio mbalimbali ya FIFA ikiwemo mashindano mbalimbali, mikutano na ziara za viongozi na wataalamu.

Kwa upande wake Rais wa FIFA Gianni Infantino amemshukuru Mheshimiwa Makonda na ujumbe wake kwa kumtembelea na kuzungumza nae na amesema FIFA ipo tayari kushirikiana na Tanzania katika programu zake za maendeleo ambazo zitasaidia kutengeneza fursa kwa vijana kunufaika na mchezo wa mpira wa miguu ikiwemo ujenzi wa miundombinu na uendelezaji wa vituo vya ufundi.

Infantino ameipongeza Tanzania kwa kazi kubwa iliyofanywa na inayoendelea kufanywa na Serikali ya ujenzi wa miundombinu ya michezo kuelekea AFCON 2027 na amesema FIFA inaunga mkono jitihada hizo.

Katika mazungumzo hayo Mheshimiwa Makonda ameongozana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa, Balozi wa Tanzania nchini Morocco Mheshimiwa Ali Mwadini, Rais wa Shirikisho la Kandanda Tanzania (TFF) Bw. Wallace Karia, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Michezo Bw. Boniface Tamba na Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa Bi. Neema Msitha.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa