Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HATA YANGA MBONA WALIWAHI KUCHUKUA WACHEZAJI WALIOTEMWA NA SIMBA!!

Na Prince Hoza Matua

KLABU ya Simba SC imemtambulisha beki wa kushoto, Nickson Clement Kibabage (25) kuwa mchezaji wake mpya akijiunga na klabu hiyo kutoka Singida Black Stars.

Kibabage alijiunga tena na Singida Black Stars msimu huu akitokea Yanga alikodumu kwa misimu miwili kati ya mwaka 2023-2025.

Alikwenda Yanga SC akitokea Singida Black Stars ambako awali alicheza kwa msimu mmoja akitokea KMC ambako alikuwa anacheza kwa mkopo kutoka Difaâ Hassani El Jadidi ya Morocco.

Kibabage alijiunga na DifaĆ¢ Hassani El Jadidi mwaka 2019 akitokea Mtibwa Sugar iliyomuibua katika timu yake ya vijana na kufanya vizuri kikosi cha kwanza msimu mmoja tu, 2018-2019 kabla ya kuuzwa Morocco kwa mkataba wa miaka minne. 

Ujio wake kwenda Simba, umezua sintofahamu nyingi hasa kutoka kwa mashabiki wengi wakiwa ni wa Yanga SC ambapo wanabeza usajili huo, inaonekana Simba imefulia kiasi kwamba inashindwa kuingia sokoni kutafuta beki mwenye uwezo mkubwa wa kucheza beki ya kushoto.

Tangu alipoondoka Mohamed Hussein Tshabalala au Zimbwe Jr aliyejiunga na Yanga, Simba inaonekana kushindwa kupata mlinzi mwingine wa kushoto hadi kuangukia kwa Kibabage.

Baada ya kuondoka Tshabalala, uongozi wa Simba ulikamilisha usajili wa beki mwingine wa kushoto Anthony Mligo kutoka klabu ya Namungo FC ya Ruangwa mkoani Lindi.

Mligo lilikuwa chaguo la kocha wa klabu hiyo Fadlu David's ambaye kwasasa ameondoka kwenye klahu hiyo na kocha wa sasa Steve Barker ajafurahishwa na kiwango chake na ametoa pendekezo asajiliwe beki mwingine wa kushoto.

Barker ameuagiza uongozi wa Simba umsajilie mabeki wawili wa kushoto mmoja akiwa ni mzawa na mwingine wa kigeni, hapo ndipo viongozi wa Simba walipoona umuhimu wa kumsajili Kibabage, kwani wanasema hakuna beki mzawa wa kushoto kama Kibabage.

Ni kweli kwamba Yanga walimtema kwa sababu wanao mabeki wawili ambao ni bora, Chadrack Boka raia wa DR Congo na mzawa Mohamed Hussein Tshabalala walitosha kumuondoa Kibabage kwenye kikosi cha Yanga.

Simba kuamua kumsajili Kibabage siyo dhambi na wala siyo kosa, kwani hata Yanga wamewahi kuwasajili wachezaji waliotemwa na Simba na waliweza kupokelewa vema na mashabiki wao.

Wanasimba wasiwe wanyonge kubezwa kwa Kibabage, kwani Simba siyo timu ya kwanza kufanya hivyo, Yanga iliwahi kumsajili Amisi Tambwe ambaye aliachwa na Simba, pia ikamsajili Jean Baleke ambaye naye aliwahi kuachwa na Simba.

Lakini haitoshi Yanga wakaendelea kusajili wachezaji wanaotemwa na Simba, kwani walimsajili Augustine Okrah, ninaamini kabisa Nickson Kibabage ni mchezaji mzuri na ataendelea kukiwasha kwenye kikosi cha Simba msimu aliojiunga nao.

ALAMSIKI



Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa