Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Azam FC yapata ushindi wa kwanza kombe la Shirikisho

TIMU ya Azam FC imetoka nyuma na kushinda mabao 2-1 dhidi ya wenyeji, Nairobi United katika mchezo wa Kundi B Kombe la Shirikisho Afrika jioni ya leo Uwanja wa Taifa wa Nyayo Jijini Nairobi.

Mshambuliaji Duncan Oluoch alianza kuifungia Nairobi United dakika ya 14, kabla ya mshambuliaji Mkongo, Jephte Kitambala Bola kuisawazishia Azam FC dakika ya 17 na kipa Mghana, Ernest Mohammed akajifunga dakika ya 78 akijaribu kuokoa kuipatia timu ya Tanzania bao la ushindi.

Azam FC inapata ushindi wa kwanza baada ya kupoteza mechi mbili mfululizo, ikifungwa 2-0 na wenyeji Maniema United huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na 1-0 dhidi ya Wydad Athletics Club ya Morocco visiwani Zanzibar.

Kwa Upande wao Nairobi United wanapoteza mechi ya tatu mfululizo ya Kundi B kufuatia kufungwa 3-0 na Wydad AC Jijini Casablanca na 1-0 nyumbani dhidi ya Maniema United.

Mchezo mwingine wa Kundi B utafuatia Saa 2:00 usiku baina ya Wydad AC na AS Maniema Union Uwanja wa Mohammed V Jijini Casablanca kabla ya timu hizo kurudiana Februari 1 Uwanja wa Martyrs Jiji
Azam FC inarejea nyumbani kujipanga kwa mchezo wa marudiano na Nairobi United Februari 1 pia Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa