Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Joseph Mwita "Jenerali Mwitakiaro": Galacha wa salamu aliyejipatia umaarufu mkubwa Afrika mashariki

Na Mwandishi Wetu

KWA Sasa ni marehemu, lakini enzi za uhai wake alijulikana sana kwenye vipindi vya salamu katika vituo kadhaa vya Afrika mashariki, kwa maana nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi ikiwemo Tanzania yenyewe.

Jina lake la kuzaliwa anaitwa Joseph, ila alijulikana kwa jina la Jenerali Mwitakiaro au baba Cevini enzi za uhai wake niliwahi kumuuliza kwanini unajiita Jenerali Mwitakiaro, akajibu Mwitakiaro alikuwa Jenerali wa jeshi la ulinzi wa Tanzania, JWTZ.

Jenerali Ernest Mwita Kiaro alipata kuwa mkuu wa majeshi ya ulinzi wa Tanzania na alifariki mwaka 1994, Joseph ambaye ni mzaliwa wa Mtwata, Kusini mwa Tanzania ni tofauti kubwa na Mwita Kiaro ambaye ni mzaliwa wa mkoani Mara, kanda ya ziwa, magharibi mwa Tanzania.

Joseph alitokea kuvutiwa na Jenerali Ernest Mwita Kiaro na akaamua kulibadili jina lak e na kujiita Mwitakiaro Joseph alikuwa kinyozi wa nywele katika mitindo mbalimbali ambayo aliiweza.

Mpaka anakutwa na mauti, alikuwa katika saluni moja iliyopo Tabata shule jirani na zahanati ya Tabata shule, kwakweli alikuwa kinyozi mzuri ambaye aliaminika na wengi kuanzia wateja zake na mabosi wa saluni.

Siku ya msiba wake, watu mbalimbali wa maeneo ya Tabata na jirani walikusanyika kumzika fundi huyo mwaminifu, ikumbukwe kwamba katika mafundi wote, kinyozi ndio mwaminifu, kwakuwa unamlipa pesa na anakupa umachokitaka kwa wakati husika.

Jenerali Mwitakiaro alianza kujiingiza kwenye salamu kuanzia mwaka  1999 na aliendelea kudumu kwenye salamu mpaka mwaka 2025 alipofariki.

Kwa maana Jenerali Mwitakiaro alijipatia umaarudu mkubwa kwenye redio za FM na AM kwa maana TBC Taifa, Radio One, Magic FM, Redio Free Africa, EAST Africa, Clouds FM, Wasafi FM, EFM, Uhuru FM, Abood FM na nyinginezo.

Marehemu Mwitakiaro ambaye amefariki akiacha watoto wawili wote wa kike ambapo mtoto mkubwa anasoma darasa la sita na mdogo wake anasoma darasa la pili, alizaliwa miaka ya 1979 na alianza salamu kwenye camp ya Pentagon yenye maskani wake Tabata Mawenzj jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa mwanasalamu mwingine aliyefanya salamu kwa ushirikiano mkubwa Nassoro Yusuph amesema Mwitakiaro alianza na Pentagon salamu Club ambapo kipindi hicho walikuwa wanatumia post card.

Yusuph anasema kipindi hicho salamu kwa njia ya post card ilikuwa Radio One, TBC Taifa ambapo wakati huo ikiitwa Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD), Uhuru FM na baadaye Magic FM, lakini mtindo wa post card ulikufa na wakahamia kwenye kupiga simu.

Kwenye club ya Pentagon, marehemu Mwitakiaro alikutana na Yusuph Nindi "Nindiboy", Chief Masanja, Mgosi wa Ndima Muya na wengineo ambao walipata umaarufu kupitia redio.

Lakini pia Jenerali Mwitakiaro alikutana na wanasalamu wengine wa miaka ya 2000 kama akina Nassoro Yusuph, Shukuru Ki Nyange, Omary K Nyange, Shabani Kipresha, Omary Rajabu, Masha Mfinanga, Athuman Mkele, Prince Hoza, Peter Toshiboy, Rajabu Magomba, Grace Michael, Hawa Hassan na wengineo ambao alifanya nao zalamu utadhani wanalipwa.

Jenerali Mwitakiaro amewahi kusafiri mikoa kadhaa hapa nchini na nchi jirani na salamu ndio iliyompeleka, mwanasalamu huyo aligharamiwa kwenda maeneo hayo kutokana na umaarufu wake kupitia redio, kifo chake kimesikitisha wengi ingawa mwenyezi Mungu alimpenda zaidi.

ALAMSIKI
Joseph Mwita "Jenerali Mwitakiaro"

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...