Ruka hadi kwenye maudhui makuu

JKT Queens mabingwa wa CECAFA

TIMU ya JKT Queens imefanikiwa kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa ya Wanawake Afrika Mashariki na Kati ya CECAFA baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda katika mchezo wa Fainali leo Uwanja wa Moi International Sports Centre uliopo Kasarani Jijini Nairobi nchini Kenya.

Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, kiungo chipukizi wa umri wa miaka 17, Winfrida Hubert Gerald dakika ya tano na hilo linakuwa taji la pili la michuano hiyo kwao baada ya lile walilotwaa mwaka 2023 nchini Uganda.

JKT Queens inajikatia tiketi ya kwenda kucheza Ligi ya Mabingwa Afrika kwa Wanawake, michuano itakayofanyika baadaye mwaka huu nchini Algeria.

Pamoja na kutwaa taji hilo, JKT Queens imetoa Mfungaji Bora ambaye ni mshambuliaji wake, Jamila Rajab aliyefunga mabao matano, akifuatiwa kwa mbali na wachezaji watatu wa Kampala Queens, Kamiyati Naigaga, Tourist Lema Tone, Peace Muduwa na Emily Kemunto wa Police Bullets na Winfrida Mathias wa JKU Princess waliofunga mabao mawili kila mmoja.

Mchezo uliotangulia wa kusaka mshindi wa tatu, bao pekee la mshambuliaji Mganda, Margaret Kunihira limewapa wenyeji, Police Bullets Medali ya Shaba baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Kampala Queens ya Uganda hapo hapo Uwanja wa Moi Kasarani.

Ikumbukwe JKT Queens iliingia Fainali baada ya kuwatoa wenyeji, Police Bullets kwa penalti 4-2 kufuatia sare ya 1-1 na Rayon Sports iliifunga Kampala Queens kwa penalti pia, 4-2 kufuatia sare ya bila mabao ndani ya dakika 120 mechi hizo zote pia zilipigwa hapo hapo Moi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...