Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AZIZI ANDABWILE NA KUPANDA NA KUSHUKA

Na Prince Hoza Matua 

KILA Mwanayanga aliyeona jina la Azizi Andabwile katika mechi hiyo ya watani wa jadi basi lazima alishtuka na kuogopa na wengine walifikia stage ya kuhoji huyo kwanini aanze lakini mwamba akaja kuwaziba midomo kwa performance bora sana.

Kiukweli mwamba kauwasha sana tena sana anafaa kuwa Man of match, lakini cha ajabu tangu mwanzo mwa mechi hadi mwishoni huku katika kibanda umiza kuna watu walikuwa wanapiga kelele wanataka atolewe sasa sijui walikuwa wanaangalia mechi tuliokuwa tunaangalia sisi au marudio.

Ujio wa kocha Roman Folz raia wa Ufaransa mwenye asili ya Morocco, umeweza kubadili upepo ndani ya kikosi cha Yanga SC msimu huu na Azizi Andabwile amechukua hatami.

Maisha ya Andabwile ni ya kupanda na kushuka, alijiunga na Yanga kimaajabu, kwani wakati anang' ara kwenye soka, hakupata nafasi ya kusajiliwa na klabu yoyote kubwa kati ya Yanga au Simba.

Mchezaji huyo aliibuliwa na timu ya Mbeya City ya mkoani Mbeya, mkoa ambao ndiko alikotokea, wakati mashabiki wengi wa soka nchini wakiamin kwamba nafasi yake ya kucheza vilabu vikubwa vitatu vya Yanga, Simba au Azam ilikuwa wakati ule, lakini bahati yake imechomoza jioni.



Andabwile ni kiungo mkabaji anayeweza kucheza vizuri namba sita, alipotea ghafla kwenye soka kabla ya Singida Black Stars kumrejesha hewani na akaanza kuchomoza upya.

Msimu uliopita Singida Black Stars walimpeleka kwa mkopo Yanga SC, ingawa hakupata nafasi kwenye kikosi cha kwanza, maisha yake ndani ya Yanga hayakuwa mazuri kwani benchi lilimtesa.

Yanga iliyonolewa na makocha tofauti akianza na Miguel Angel Gamondi raia wa Argentina, Sead Ramovic raia wa Ujerumani na Miloud Hamdi raia wa Algeria, wote hawakumpa nafasi kutokana na ubora wa Khalid Aucho.

Ni ngumu kwa kocha yoyote kumuweka nje Aucho na kumfikiria Andabwile, mchezaji huyo aliendelea kukaa benchi hata kama Aucho hachezi, kwakuwa Yanga ilikuwa na namba sita mwingine Jonas Mkude ambaye naye alikuwa na kiwango bora.

Licha ya nyota hao wawili, Aucho na Mkude) kuondoka kwenye kikosi hicho, kuelekea mchezo wa dabi, Yanga na Simba kuwania Ngao ya Jamii, jina la Duke Abuye lilikuwa linatajwa kwenye namba sita.

Wachambuzi wengi wa soka walienda na jina la Duke wakidhanj Kwamba ataanza kwenye kikosi hicho akichukua nafasi ya Aucho, lakini ndivyo sivyo, kocha Roman Folz alimwanzisha Andabwile.

Roman alianza kumuamini Andabwile tangia alipoanza kukinoa kikosi cha Yanga mwanzoni mwa msimu huu akichukua mikoba ya Miloud Hamdi, Andabwile aliaminiwa kwenye mchezo wa kirafiki wa kimataifal dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda mchezo uliofanyika uwanja wa Amahoro mjini Kigali.

Katika mchezo huo Yanga SC ikishinda mabao 3-1, Andabwile alijifunga, lakini mashabiki wa Yanga walimsamehe wakiamin kwamba kujifunga kwake kulitokana na kukaa kwake benchi muda mrefu hivyo kulimuondolea kujiamini.

Lakini Folz aliendelea kumuamini kwenye mechi nyingine za kirafiki, kwenye mchezo wa watani hakuna aliyedhani kama Folz atamuanzisha kwani historia ya mechi hiyo kila timu hupanga wachezaji wanaoaminika, mimi mwenyewe nilijua Duke ataanza kama namba sita wa moja kwa moja.

Kwa jinsi alivyocheza kwenye mchezo huo na timu yake ikishinda, sidhani kama kocha atamweka nje katika michezo ijayo, tutegemee kimuona Andabwile kwenye mchezo dhidj ya Willete ya Angola.

ALAMSIKI


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...