Rasmi, Simba yakataa kucheza Ngao na Yanga Septemba 16

“Kusema ukweli ukijaribu kuangalia ratiba imekuwa ngumu Sana  maana ratiba ya Ngao ni tarehe 16, kuanzia hapo tutakuwa na Siku tatu au nne inabidi tucheze mchezo wa ligi ya mabingwa Botswana, na kama unavyojua utaratibu wa kusafiri Botswana Huwa ni magumu sana na mara nyingi Huwa tunaenda na Ndege ya kukodi kuepusha usumbufu”

Lakini ukijaribu kuangalia ucheze mechi tarehe 16, hapo hapo inabidi upumzike , halafu usafiri na baadae kati ya tarehe 19 au 20 ucheze Mchezo Unaweza kuona ni kwa Kiasi Gani ni vigumu”

“Kama Mchezo utakuwa tarehe 20 angalau naona Kuna namna tunaweza kukimbizana na mambo lakini kama wenyeji wetu watachagua tarehe 19 basi ratiba itazidi kuwa ngumu zaidi”

Meneja wa habari na mawasiliano wa Simba SC Ahmed Ally akizungumza na E fm Leo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI