Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Albamu yangu ya NJE NDANI nilifanya nje ya nchi- Mr Sugu

"Albamu yangu ya NJE YA BONGO nilifanyia Nje ya nchi mwaka 1999, na ndio albamu yangu ya kwanza kuisambaza mwenyewe.

Big up kwa Mzee Kitime maana ndiye alinisaidia kusambaza albam yangu ya kwanza kabla ya albamu ya pili na ya tatu hazijachukuliwa na promota Mutta.

Baada ya kutoridhika na mwenendo mzima wa biashara niliamua kuisambaza mwenyewe.

Sasa, nikiangalia kila wanao-duplicate (durufu) ni wadosi, mahali pekee ambapo ningeweza ku-duplicate ni CHAMUDATA (Chama cha Muziki wa Dansi Tanzania)

Wao walikuwa na sponsorship kutoka Norway chini ya Mzee John Kitime akiwa kama Katibu, pale walikuwa na studio na chumba kwa ajili ya ku-duplicate tapes.

Nilimfuata Mzee Kitime nikamwomba ni-duplicate albamu yangu, akasema b'ana ili uwe mnufaika lazima uwe member.

Wakati huo hatukuwa na Chama cha Rap ilibidi mimi niwe Mwanachama wa CHAMUDATA!

Kwa hiyo, mimi nimewahi kuwa member wa CHAMUDATA, big up kwa brother Kitime kwa sababu yote hii alikuwa anatafuta namna ya kunisaidia." Joseph Mbilinyi, Sugu.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa