Simba na Yanga kukutana tena Arusha, Samia Super Cup

Mkuu wa mkoa wa Arusha, Paul Makonda amealika timu nne za soka la wanawake kushiriki michuano ya Samia Suluhu Hassan Super Cup 2025 itakayoanza kutimua vymbi Machi 4 hadi 6.

Timu zilizopokea mualiko ni JKT Queens, Fountain Gate Queens, Simba Queens na Yanga Princess.

Timu hizo zitaanza kwa kucheza nusu fainali tarehe 4 na kufuatiwa na fainali tarehe 6.