Chippa United yamtema Majogoro

Kiungo wa timu ya taifa ya Tanzania Baraka Majogoro ameachana na klabu yake ya Chippa United kwa makubaliano ya pande zote mbili.

Majogoro (27) ambaye alijiunga na miamba hiyo ya Afrika Kusini mnamo Agosti 2023 akitokea KMC Majogoro amekosa mechi tano tu kwenye michuano yote klabuni hapo msimu huu.

Nyota huyo wa zamani Ndanda Fc, Polisi Tanzania na Mtibwa Sugar kwa sasa ni mchezaji huru na upo uwezekano wa kuendelea kukipiga Afrika Kusini huku vilabu kadhaa vikitajwa kuhitaji saini yake.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI