Simba ni nzuri kuliko Yanga- Ahmed Ally

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally amesema timu yao ni nzuri kuliko ypyote katika ukanda huu wa Afrika mashariki, ina maana Simba ni nzuri kuliko Yanga.

"Timu yetu ni bora kuliko timu nyingine yoyote kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, timu yetu imeimarika sana

Mwanasimba inabidi ujivunie timu yako maana ubora wa kikosi unaongezeka siku hadi siku

Mchezo wa Jumapili lazima kila Mwanasimba ajue umuhimu wake maana mpinzani tunayekutana nae anataka kufufukia kwetu na sisi hatuko tayari kuona CS Sfaxien anafufukia kwetu

Hakuna ambaye amewahi kupata uhai ndani ya Uwanja wa Benjamin Mkapa."

Semaji Ahmed Ally


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA