MO Salah kutimka mwishoni mwa msimu

Nyota wa Liverpool raia wa Misri Mo Salah amesema anakaribia kuondoka klabuni hapo kutokana na mkataba wake kufikia ukingoni

“Tayari tunaikaribia Disemba lakini sijapokea ofa yeyote mpaka sasa ya kuongeza mkataba na kuendelea kusalia hapa , naipenda sana Liverpool nawapenda mashabiki wake na kwangu mimi haijawahi kutokea klabu bora kama Liverpool lakini mwisho wasiku hili lipo nje ya uwezo wangu’’ Mo Salah

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 32 mkataba wake utafika tamati Juni 2025 alijiunga na Liverpool 2017 akitokea AS Roma mpaka sasa ameisaidia klabu yake kubeba EPL 2020, UCL 2019 na msimu huu amecheza mechi zote 12 ndani ya EPL huku akifunga magoli 10 na assist 6 na kuiweka klabu yake kileleni mwa msimamo wa ligi.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI