Gamondi kumrithi Aussems, Singida Black Stars

Baada ya klabu ya Singida Black Stars kumfungashia virago kocha wake mkuu Patrick Aussems pamoja na msaidizi wake Denis Kitambi, tayari klabu hiyo imeanza mazungumzo na makocha kadhaa ili kurithi nafasi hiyo.

Kocha aliyefurushwa na Yanga SC hivi karibuni, Miguel Gamondi raia wa Argentina anatajwa kuwa kwenye rada za klabu hiyo na ikiwezekana atarejea tena kwenye ligi hiyo kuendelea na majukumu yake.

Yanga ilimfuta kazi Gamondi baada ya kupoteza michezo miwili dhidi ya Azam FC na Tabora United, Wanangwani hao waliamua kumtimua kazi Gamondi na msaidizi wake Moussa Ndaw raia wa Senegal, Yanga ikifungwa 1-0 na Azam FC na 3-1 na Tabora United.

Miguel Gamondi

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI