Yanga haina majeruhi yoyote
Meneja wa kikosi Cha Yanga SC Walter Harrison amesema hakuna majeruhi yoyote kwenye kikosi chao zaidi ya Farid Mussa ambaye ameanza mazoezi.
Kwa mujibu wa maneno ya Harrison, zinaondoa taarifa za kuumia Ibrahim Baka, kwamba watu waliovumisha kwenye Instagram hazina ukweli wowote.
"Wachezaji wote waliokua kwenye majukumu ya timu za Taifa wapo vizuri,hakuna taarifa mpya kuhusu majeraha zaidi ya Farid Mussa ambaye ameanza mazoezi mepesi,wengine wote wapo sawa"Walter Harrison Meneja wa kikosi cha Yanga.