Samatta awajaza matumaini Watanzania kufuzu AFCON
Nyota wa timu ya Taifa ya Tanzania Mbwana Ally Samatta baada ya mchezo dhidi ya DR Congo waliopoteza 2-0 uwanja wa Taifa ameonyesha kuwa bado ana matumaini na timu ya Taifa.
" Ipo siku vijana watakuwa bora na kutupa furaha wa-Tanzania."
- Mbwana Samatta.
Nyota huyo licha ya kuumia kwenye mchezo huo lakini hakujali aliendelea kuipigania bendera ya nchi kwa moyo na jasho lake lote.
Stars imesaliwa na michezo miwili kwenye kampeni ya kufuzu fainali za mataifa ya Afrika dhidi ya Guinea na dhidi ya Ethiopia.