Nyota wa Simba SC ataka lawama zote Taifa Stars apewe kocha na si wachezaji
Mchezaji wa zamani wa Simba SC na kocha wa Friends Rangers Said Msasu amewataka wapenzi na mashabiki wa soka nchini kutowalaumu wachezaji wa timu ya taifa, Taifa Stars kutokana na kipigo cha mabao 2-0 toka kwa DR Congo na isipokuwa lawama zote zipelekwe kwa benchi la ufundi la timu hiyo.
"Sio sahihi wakulaumiwa ni benchi la ufundi walitakiwa liwe na game plan kila mechi ina uchezaji wake away na home na aina ya wachezaji na line up na sub haiwezekani tunatafuta goli inafanyika sub ya kutoa", alilalamika Msasu.