Mohamed Salah agomea uwanja wa nyasi bandia
MSHAMBULIAJI wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri, Mohamed Salah ameripotiwa kurejea England kwa kuwa hatocheza mchezo wa kesho dhidi ya Mauritania kwa sababu uwanja unaotumika umetengenezwa kwa nyasi bandia.
.
Taarifa ya FA ya Misri ilisema: “Benchi la ufundi likiongozwa na meneja Hossam Hassan walifanya mazungumzo na Mohamed Salah na wakaafikia kumpumzisha kwenye mechi ijayo sababu hali ya kiwanja na uchezaji wa Mauritania vinaweza kumsababishia majeraha.”
.
Mchezo huo wa kesho unatarajiwa kupigwa kwenye uwanja wa Cheikha Ould Boidiya wenye uwezo wa kuingiza watu 8,200 ambao unapatikana jijini Nouak-chott.