Ibrahim Baka kuikosa Simba Jumamosi
Kuna uwezekano mkubwa beki wa kati wa mabingwa wa soka nchini Yanga SC Ibrahim Hamad "Baka" ataukosa mchezo wa watani dhidi ya Simba SC utakaochezwa Jumamosi uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam.
Akipost kwenye mtandao wake wa Instagram, Baka ameandika kwamba ameumia katika mchezo wa kufuzu AFCON dhidi ya DR Congo ambapo timu ya taifa ya Tanzania ilifungwa mabao 2-0.
Kukosekana kwake kwenye mchezo huo kunaweza kuwa pengo kubwa kwa Yanga ambao watakuwa wageni wa Simba katika mchezo huo ambao wanataka kulipa kisasi cha kufungwa mechi tatu mfululizo