Gamondi awaandalia mvua ya magoli Simba
Kocha wa Yanga SC Miguel Gamondi raia wa Argentina amesema watacheza kwa nidhamu kubwa kuwaheshimu wapinzani wao Simba SC Jumamosi lakini anawaandaa vijana wake kushinda kwa idadi kubwa ya magoli.
“Simba ni timu kubwa yenye wachezaji wenye vipaji vikubwa na historia ya mafanikio. Tunawaheshimu sana kama wapinzani, lakini tunajipanga vizuri kwa mchezo huu.
.
“Tunafahamu wanavyocheza na nguvu yao, lakini tutatumia maandalizi yetu kuleta ushindani na kuhakikisha tunapata matokeo mazuri kwa kutumia nafasi kufunga mabao.”