Duchu alikubali benchi
Beki wa kulia wa Simba David Kameta ‘Duchu’ amesema kama mchezaji anatamani kucheza lakini mchezaji anaepata nafasi ya kucheza mara kwa mara Shomari Kapombe anatekeleza vizuri majukumu kwenye eneo lake ndio maana anaendelea kucheza mara kwa mara.
Duchu ameongeza kuwa bado hajakata tamaa, anaamini ipo siku ataaminiwa na kupewa nafasi ya kucheza mara kwa mara.
Eneo la ulinzi wa kulia la Simba lina wachezaji watatu, Shomari Kapombe, David Kamera ‘Duchu’ na Kelvin Kijili lakini hadi sasa bado chaguo la Kocha wa timu hiyo Fadlu Davids kimekuwa kwa mkongwe Kapombe na mara kadhaa Kijili amepata nafasi kwenye kikosi cha Simba.