Diamond Platnumz ajitabiria kifo chake
MwimbajiDiamondPlatnumz amefunguka baada ya yote ambayo yanaendelea mitandaoni. Kupitia insta story yake leo, Chibu ameweka picha iliyoambatana na wimbo wa Drake “Legend” toka kwenye Mixtape yake “If Your Reading This It’s Too Late” ya mwaka 2015.
Ujumbe alioukusudia Diamond Platnumz toka kwenye mistari ya ngoma hiyo ni kwamba, hata siku akifariki na kuondoka duniani, anachokifahamu ni kwamba yeye ni Legend na ameacha alama kwa sababu ni kijana mdogo ambaye anaiwakilisha nchi.