Clara Luvanga azidi kung' ara Saudi Arabia
Mchezaji wa Tanzania, Clara Luvanga usiku wa jana ameiwezesha timu yake ya Al Nassr FC ya Saudi Arabia kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Al Amal katika mchezo wa Ligi Kuu.
Kwenye mchezo huo Clara amefunga goli moja, ikumbukwe Clara alikuwa anaichezea Yanga Princess ya Tanzania na timu ya taifa, Twiga Stars.