Cedric Kaze amfuata Nabi Kaizer Chief
Klabu ya Kaizer Chiefs imemtambulisha rasmi Cédric Kaze kama kocha msaidizi wa klabu hiyo akiungana na kocha Nasreddine Nabi ambae ni kocha mkuu wa klabu hiyo.
Wawili hao walikuwa pamoja kwenye klabu ya Yanga na wakaiwezesha kushinda mataji mawili ya ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania bara.
Kukutana tena Kaizer Chief kunaweza kuisaidia timu hiyo kurejea kwenye ubora wao kama ilivyokuwa kwa Yanga.