Yanga kuanza kumtambulisha Prince Dube
Maandalizi juu ya kumtambulisha mshambuliaji wa kimataifa wa Zimbabwe Prince Mpumalelo Dube kwenye klabu ya Yanga- yameanza sasa.
Mmoja kati ya mtu wa karibu wa klabu hiyo ameitonya Mambo Uwanjani Blog kuwa Yanga inataks kumtambulisha Dube muda wowote hivyo mashabiki wao wakae mkao wa tayari.
Dube alikuwa anaichezea Azam FC na aliamua kuvunja mkataba wake hasa baada ya kutoridhishwa na hali ya mambo, na Yanga- imekuwa timu pekee iliyomvutia na akitaka kujiunga nayo