Saido Ntibanzokiza atupiwa virago Simba
Kiungo mshambuliaji Saido Ntibazonkiza hatokuwa sehemu ya kikosi cha Simba kwa ajili ya msimu wa 2024/25 baada ya kumaliza mkataba wake.
.
Taarifa iliyotolewa mapema leo, Saido hatoonekana msimu ujao kwenye kikosi cha Simba ingawa alikuwa kwenye msimu bora, hasa wa 2022/2023 ambapo aliweza kuwa mfungaji bora.
Hata hivyo Saido anatajwa kujiunga na Coastal Union ya Tanga ambao nao watashiriki kombe la Shirikisho barani Afrika msimu ujao ambapo Simba nao watashiriki michuano hiyo hiyo