Luis Miquissone aungana na Saido
Klabu ya Simba SC imeachana na aliyekuwa Kiungo Mshambuliaji wake,Luis Miquissone kufuatia kiwango kibovu alichoonyesha nyota huyo tangu amesajiliwa na Simba kwa mara ya pili.
Miquissone hajafunga goli lolote akiwa na Simba ndani ya Mechi 19 alizocheza huku akitoa assist 4 pekee.
Jana mtandao huu uliandika kwamba Miquissone ataendelea kusalia kwenye kikosi hicho, lakini leo klabu yake ya Simba imempa thank you.