Joash Onyango kutimkia Dodoma Jiji
Na Salim Fikiri Jr
Mlinzi wa kati wa Singida Black Stars zamani Ihefu SC Joash Onyango anakaribia kujiunga na walima zabibu wa Dodoma Jiji.
Taarifa ambazo hazina shaka yoyote na chanzo chetu cha habari zimetuweka wazi kwamba Onyango raia wa Kenya ambaye aliwahi kuzichezea Gor Mahia ya Nairobi nchini Kenya na Simba SC ya Dar ea Salaam ya Tanzania, atajiunga na Dodoma Jiji msimu ujao.
Onyango amekuwa kwenye kiwango kizuri tangu alioojiunga na timu hiyo iliyokuwa ikijulikana kama Singida Big Stars kabla ya kubadilisha jina na kuitwa Singida Fountain Gate na baadaye Ihefu ikauzwa na nusu ya wachezaji wa Singida Fountain Gate wakaingia Ihefu