YANGA NA MASHUJAA KESHO MTOTO HATUMWI DUKANI
Na Ikram Khamees. Kigoma
Kesho ndio kesho katika uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma mabingwa watetezi wa Ligi Kuu bara inayodhamimiwa na benki ya NBC, Yanga SC watakapokuwa uwanjani dhidi ya wenyeji wao Mashujaa FC.
Mchezo huo unatazamwa kuwa mkali na wa upinzani hasa kwakuwa kila timu inamahitaji yake, Yanga inayoongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 62 na inahitaji kushinda ili itangaze ubingwa mapema jambo ambalo litakuwa gumu kwa Mashujaa kuiona Yanga ikitwaa ubingwa mikononi kwao.
Mashujaa nao wapo nafasi mbaya kwani sasa wanashika nafasi ya 14 wakiwa na pointi 23 hivyo wanataka kushinda ili wafikishe pointi 26 ambazo zitawashusha Geita Gold na Ihefu.
Jioni ya leo Yanga wamefanya mazoezi kabambe kujiandaa na mchezo huo wa kesho