WAWILI TWIGA STARS KESHO KUKIWASHA UTURUKI
Mastaa wawili wa timu ya Taifa ya wanawake, Twiga Stars, Opah Clement pamoja na Diana Lucas kesho watashuka dimbani kwenye Ligi Kuu ya wanawake nchini Uturuki katika michezo ya raundi ya 30 ya ligi ambayo itatamatisha msimu wa 2023/2024 nchini humo.
Timu za wachezaji hao wote wawili, Besiktas W ya Opah Clement na Amed SK W anayoichezea Diana Lucas zipo kwenye eneo salama ambalo linazihakikishia timu hizo kuwepo kwenye ligi kuu msimu ujao.