Joseph Guede hatihati kubaki Yanga

Mshambuliaji wa Yanga SC Joseph Guede amethibitisha kuwa mkataba wake na Yanga unamalizika Mwezi June mwaka huu lakini Hatma ya yeye kusalia kwenye Kikosi cha Yanga anamuachia Rais wa Yanga Engineer Hersi Said.

Guede ambae alijiunga na Yanga wakati wa Dirisha dogo la usajili 2023/2024 alisaini kandarasi ya miezi sita ndani ya viunga vya Jangwani.

Guede amethibitisha hayo wakati akifanya mahojiano na Crown Media wakati wa sherehe za Ubingwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es Salaam.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI