AL AHLY YAICHINJA SIMBA NYUMBANI

Timu ya Al Ahly ya Misri usiku huu imeifu ga Simba SC ya Tanzania bao 1-0 katika uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam mchezo wa robo fainali Ligi ya mabingwa Afrika.

Kwa matokeo ya mchezo huo, Simba sasa inatakiwa kushinda zaidi ya bao moja pasipo kiruhusu bao ili iweze kutinga nusu fainali.

Bao lililoizamisha Simba mbele ya mashabiki wake lilifungwa na Ahmed Kouka dakika ya 5 kipindi cha Kwanza.

Kesho katika uwanja huo huo Yanga wataikaribisha Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini hatua ya robo fainali



Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI