Kiungo Mshambuliaji wa Zamani wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga, Mubarak Amza Ngamchiya raia wa Cameroon amejiunga na Klabu ya Kagera Sugar ya hapa mkoani Kagera kwa mkataba wa iiaka miwili akitokea klabu ya Ihefu SC kwa uhamisho huru baada ya kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba na klabu hiyo kutoka wilayani Mbarali Jijini Mbeya.
SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
