Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MTANZANIA KUWANIA UBINGWA WA WBC UTURUKI

Bondia Pius Mpenda a.k.a 'Super Hero' kutoka Naccoz gym chini ya kocha wake Rama Jah tarehe 29/10/2023 anatarajiwa kupanda ulingoni kwenye pambano la kimataifa nchini Uturuki.

Wastani wa Mpenda kwenye mapambano yake ya kimataifa nnje ya mipaka ya Tanzania umekuwa mzuri amecheza jumla ya mapambano matatu ya kimataifa ameshinda mawili na kupoteza moja na amefanikiwa kutwaa mkanda mmoja wa dunia wa WBU.

Mpenda atacheza na bondia Dauren Yeleussinov mzaliwa wa jiji la Kayindy nchini Kazakhstan ila ni mkazi wa jiji la Brooklyn, New York nchini Marekani.

Mpenda na Yeleussinov watacheza pambano la raundi 10 ubingwa wa WBC (World Boxing Council Peace Super Welterweight kg 69 title) litakalo fanyika kwenye ukumbi wa Hilton Double jijini Instanbul nchini Uturuki.

Mpinzani wake Mpenda bondia Yeleussinov alianza safari yake ya mchezo wa masumbwii kupitia ngumi za Amateur (Ngumi za Ridhaa) tarehe 17/12/2005 dhidi ya bondia Ruslan Safiullin raia wa Kazakhstan kwenye pambano la raundi 4 na bondia Yeleussinov aliweza kushinda pambano hilo kwa matokeo ya point .

Mpaka anatoka kwenye ngumi za Amateur alikuwa na rekodi yakucheza jumla ya mapambano 37, kashinda 26, kwa "KO'S" 1, kapoteza 11 na sare 0.

Aliingia kwenye ngumi za Kulipwa (Professional Boxing) tarehe 3/12/2014 dhidi ya bondia Anthony Dwayne raia wa Marekani kwenye pambano la raundi 4 na bondia Yeleussinov aliweza kushinda pambano hilo kwa matokeo ya "TKO" kwenye raundi ya kwanza.

Mpaka sasa ni bondia mwenye hadhii ya nyota moja anacheza kwenye uzani wa Super Welterweight Kg 69 anashikilia nafasi ya 342 kati ya mabondia 1898 Duniani na nafasi namba 2 kati ya mabondia wa 5 wanaocheza uzito huo wa kg 69 nchini kwao Kazakhstan.

Akiwa na rekodi yakucheza jumla ya mapambano 14, Kashinda 11, Kwa "KO'S" 10, kapoteza 2 na sare 1.

Mpenda ni bondia mwenye hadhii ya nyota mbili anacheza kwenye uzani Middleweight kg 72 anashikilia nafasi ya 114 kati ya mabondia 1551 Duniani na nafasi namba 1 kati ya mabondia 28 wanaocheza uzito huo wa kg 72 hapa nyumbani Tanzania.

Akiwa na rekodi yakucheza jumla ya mapambano 8, kashinda 7, kwa "KO'S" 4, kapoteza 1 na sare 0.
Tunamtakia maandalizi mema bondia Pius Mpenda iliaweze kuipeperusha bendera ya Tanzania vyema.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa