WINGA ANAYETAKIWA SIMBA, AKIRI YEYE NI YANGA DAMU

Winga wa timu ya Power Dynamos ya Zambia Joshua Mutale ameweka wazi kwamba yeye ni Yanga kwa sababu alifurahishwa na mafanikio ya timu hiyo na kuamua kuvaa jezi zao.

Mutale anahusishwa kujiunga na Simba SC hasa baada ya kuichachafya timu hiyo katika mchezo wa kwanza wa Ligi ya mabingwa Afrika uliofanyika Ndola, Zambia na timu hizo kufungana mabao 2-2.

Winga huyo alikutwa amevaa jezi za Yanga katika ukurasa wake wa istagram, lakini alipoulizwa kwanini amevaa jezi ya Yanga huku yeye akotakiwa na mahasimu wao wakuu, amedai aliipenda Yanga kutokana na soka lao la kuvutia, pia anekiri kutaka kuja kucheza Tanzania ingawa hajaitaja Simba wala Yanga










Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Kocha Simba anataka wachezaji wapya watano

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI