Na Ikram Khamees
Licha ya kupata ushindi wa mabao 2-0 JKU imeondolewa katika michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika hasa baada ya kufungwa kwa jumla ya mabao 4-3 na timu ya Singida Fountain Gate.
Bahati haikuwa yao vijana wa JKU ambao kipindi cha kwanza walicheza vizuri na kufanikiwa kuongoza mabao 2-0 lakini kipindi cha pili Singida Fountain Gate walibadilika na kuzuia wasifungwe bao la tatu ambalo lingewaondoa mashindanoni.