Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HONGERA RAIS MWINYI KWA KURUDISHA MASUMBWI ZANZIBAR

Na Prince Hoza

HII mara yangu ya pili kumpongeza Rais wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hussein Ally Mwinyi kwa kurudisha mchezo wa masumbwi, lakini leo nipo tofauti na mara ya kwanza nilipoandika pongezi kwa kurudisha mchezo huo. 

Pongezi za mara ya pili ni kwa mchezo huo kuchezwa rasmi visiwani humo, wakati Serikali ya Mapinduzi ikitangaza kuurudisha mchezo huo, imechukua mwaka sasa hakuna pambano lolote lililowahi kufanyika. 

Agosti 27 kuliandaliwa pambano la masumbwi lililowakutanisha mabondia kutoka Zanzibar na Tanzania bara, kufanyika kwa pambano hilo ambapo ni baada ya miaka 60 bila radhaa ya mchezo wa masumbwi hatimae historia ya ngumi kutoka visiwani Zanzibar imerejea. 

Kampuni ya Tosh Sports Promotion kwa kushirikiana na Kamisheni ya ngumi visiwani Zanzibar pamoja na Azam Media Limited imeuleta mchezo wa ngumi Zanzibar kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi. 

Zanzibar na Tanzania bara kwa ujumla imeshuhudia usiku wa kipekee wa ngumi kwa pambano kuu la bondia Ibrahim Class Mgender a k a King Class Mawe dhidi ya Hamis Muathai walioandika historia ya kwanza ya ufunguzi wa mchezo wa masumbwi visiwani Zanzibar. 

Mabondia Class na Hamisi watacheza pambano la raundi 8 kwenye uzito wa lightwigh kg 61 lisilo la ubingwag. 

Class anarudi kwenye pambano hili tangu alivyocheza pambano lake la mwisho hapa jijini Dar es Salaam tarehe 25/5/2023 dhidi ya mpinzani wake Said Chino a k a Bull Dog. 

Pambano la ubingwa wa taifa kwenye uzito wa Super Featherweight kg 58 na alifanikiwa kushinda pambano hilo kwa majaji wote watatu. 

Pia kutakuwa na mapambano mengine ya utangulizi yaliyo sherehesha rasmi kurejea kwa ngumi katika visiwa vya Zanzibar mabondia kama Karim Mandonga na Dullah Mbabe walikuwepo kwenye mapambano hayo yatakayofanyika kwenye uwanja wa Mao Tse Sung visiwani Ungujo ndipo yalipigwa mapambano yote. 

Class alienda kwenye pambano hilo akiwa na rekodi ya jumla ya mapambano 36 kashinda 30 kwa ko 14 kapoteza 6 na sare 0, historia iliandikwa Agosti 27. 

Bila shaka natumia nafasi hii tena kumpa hongera Rais huyu wa Zanzibar kwani wamepita Marais sita kushindwa kuurejesha mchezo huo.

Rais wa awamu ya kwanza wa Zanzibar Abeid Amaan Karume ndie aliyeupiga marufuku mchezo huo mwaka 1963 hasa baada ya Uhuru kutoka kwa Uingereza na Sultan wa Oan aliyeitawala kwa rane kadhaa zilizopita.

Rais Karume aliuzuia mchezo huo akidai hauna maana yoyote na ni mchezo wa kitumwa kwani wakoloni waliwashindanisha watumwa ili kupata mlo au kitu chochote hivyo watumwa pekee waliingia ulingoni huku mkoloni akikaa kwenye kiti kuangalia mpambano.

Hivyo Karume alipofanikiwa kuikomboa Zanzibar akasitisha mchezo huo, Rais Mwinyi amekuwa Rais wa kwanza kuurudisha mchezo huo baada ya Uhuru. 



ALAMSIKI

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa