ROMA AMKANA NEY WA MITEGO

Msanii wa Hip Hop, Roma amelitaka Baraza la Taifa (Basata) kumbana Nay wa Mitego yeye mwenyewe kuhusu wimbo wake mpya, Amkeni.

Kauli ya Roma inakuja baada ya Nay kudai baadhi ya mistari ya wimbo huo alipatiwa na Roma kitu ambacho amekikanusha.

"Sijamtumia kitu chochote wala sijahusika kwenye wimbo wake huo, kwanza hata namba yake ya simu sina, ananisingizia na sijapenda!."

"Akija hiyo Jumatatu, malizaneni naye pekee yake, mimi nina familia na watoto wananitegema kupitia huu muziki, sitaki hekaheka sasa hivi." ameandika Roma.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI