KOCHA WA MASHUJAA AFUNGIWA MSIMU MZIMA

Kocha wa Magolikipa wa timu ya Mashujaa FC Shomari Ndizi amefungiwa kwa msimu mzima wa 2023/24 kushiriki michezo yote ya ligi na mashindano yote yaliyo chini ya TFF na pia ametozwa faini ya Tsh Milioni mbili kwa kosa la kumpiga ngumi usoni kocha Mkuu wa klabu ya Mbeya City Abdallah Mbiru wakati wachezaji wa akiba na benchi la ufundi la Mashujaa wakishangilia bao walilofunga kwenye mchezo wa mtoano wa mkondo wa pili wa kuwania kucheza ligi kuu uliochezwa jijini Mbeya.

Adhabu hii ni kwa kuzingatia kanuni ya 45:2(2:1) ya championship kuhusu udhibiti wa makocha.




Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI