WYDAD CASABLANCA YAITOA SIMBA NA KUTINGA NUSU FAINALI

Na Prince Hoza

Mabingwa watetezi wa Ligi ya mabingwa barani Afrika, Wydad Casablanca ya Morocco usiku huu imefanikiwa kutinga nusu fainali baada ya kuifunga Simba SC ya Tanzania mabao 4-3 kwa mikwaju ya penalti kutokana na sare ya 1-1 ndani ya dakika 180.

Katika mchezo wa leo Wydad ilipata ushindi wa bao 1-0 na kufanya timu hizo kufungana 1-1 kwani Simba nayo ilipata ushindi wa bao 1-0 katika uwanja wake wa nyumbani wa Mkapa jijini Dar es Salaam.

Mchezo wa leo umefanyika katika uwanja wa Mohamed wa 5 uliopo mjini Casablanca ambapo Bouly Sambou alifunga goli pekee la ushindi lililopelekea timu hizo kupigiana penalti.

Shomari Kapombe na Clatous Chama ndio wachezaji wa Simba waliopoteza mikwaju ya penalti, Simba sasa wameshindwa kufika nusu fainali na kama kawaida yao kutolewa kwenye hatua ya robo fainali





Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI