Ndanda yajitoa Ligi daraja la kwanza bara

NDANDA WAKUBALI YAISHE

Klabu ya Ndanda ya Mtwara imetangaza kujitoa katika Ligi Daraja la Kwanza (Championship), huku sababu ikielezwa ni ukata kiasi Cha kushindwa kumudu gharama za kujiendesha.

Timu hiyo ilipaswa kusafiri kuelekea mkoani Mwanza kwa ajili mchezo dhidi ya COPCO Veteran lakini walikosa fedha za kugharamia safari hiyo.

Baada ya hali hiyo Uongozi umetangaza kujitoa rasmi kwenye Ligi hiyo huku ukisisitiza walijaribu kuwashirikisha wadau mbalimbali ili wapate msaada lakini ilishindikana.

Ndanda inakuwa ni timu ya pili msimu huu kujitoa katika Ligi Daraja la Kwanza (Championship) baada timu ya Gwambina kufanya hivyo katikati ya Msimu wa Ligi.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI