AZAM FC WAJINASIBU KUFANYA VIZURI MSIMU UJAO AFRIKA

Uongozi wa klabu ya Azam FC ‘Wanalamba lamba’ umesema, watahakikisha msimu ujao wa mwaka 2023-24 wanafanikiwa kufanya vizuri kwenye mashindano ya kimataifa kwa kutinga hatua ya makundi ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika.

Mkurugenzi Mtendaji wa klabu ya Azam FC, Abdulkarim Amin ‘Popat’ ameiambia EATV kuwa, mpaka sasa wameshajihakikishia nafasi ya ushiriki wa kombe la shirikisho barani Afrika hivyo wanaendelea kuweka mipango ya kuboresha benchi la Ufundi na wachezaji.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI