URUGUAY YAIKUNG' UTA URUSI 3-0, SAUDI ARABIA YAIUMBUA MISRI NA SALAH WAO HADI HURUMA

Mabao matatu yaliyofungwa na Luis Suarez dakika ya 10, Denis Sheryshev dakika ya 23 na Edison Cavani dakika ya 90 yametosha kuipa ushindi wa mabao 3-0 Uruguay dhidi ya wenyeji Urusi na kuwafanya waibuke vinara kundi A.

Matokeo hayo yamewafanya kufikisha pointi 9 ikishika nafasi ya kwanza, mchezo mwingine Saudi Arabia i imeizamisha Misri mabao 2-1 na kuwafanya wafikishe pointi tatu huku Misri ikiwa timu iliyotia aibu kwenye kundi A ikifungwa mechi zote tatu na kurudi bila hata pointi moja, mabao ya Saudi Arabia yamefungwa na Salman Al Faraj dakika ya 45 na Salem dakika ya 90 wakati lile la Misri lilifungwa na Mohamed Salah dakika ya 22.

Usiku huu kutapigwa mechi nyingine mbili Ureno na Iran wakati Hispania na Morocco

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI