MTIBWA SUGAR YAIBOMOA KAGERA SUGAR

Na Ikram Khamees. Dar es Salaam

Timu ya Mtibwa Sugar ya Morogoro imeibomoa Kagera Sugar baada ya kumnasa kiungo mshambuliaji Jaffar Kibay kwa kumsainisha mkataba wa miaka miwili.

Usajili huo ni sehemu ya kukiimarisha kikosi hicho kwa ajili ya msimu ujao pia ni matayarisho yake kwa ajili ya kushiriki michuano ya kimataifa mwakani.

Akizungumzia usajili huo Afisa habari wa Mtibwa Sugar, Tobias Kifaru amesema ujio wa Kibaya ndani ya kikosi hicho ni kama amerejea tena nyumbani kwani aliwahi kuichezea Mtibwa kabla hajajiunga na Kagera Sugar

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI