Kaseja adaiwa kujiunga na KMC

Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam

Mlinda mlango wa Kagwra Sugar Juma Kaseja anadaiwa amemalizana na uongozi wa timu iliyopanda Ligi Kuu Bara KMC yenye maskani yake Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Taarifa za Kaseja kutua KMC zinasema kuwa kipa huyo amesaini mkataba wa miaka miwili na ataitumikia timu hiyo msimu ujao, Kaseja ni mali ya KMC kwani hakuwa na mkataba wa Kagwra Sugar alikuwa anacheza tu kilisema chanzo chetu cha habari.

Kaseja ni kipa mkongwe hapa nchini aliyepata kuzichezea Simba na Yanga pamoja na Mbeya City pia aliwahi kuichezea Moro United na timu ya taifa,Taifa Stars kwa nyakati tofauti

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI