Ruka hadi kwenye maudhui makuu

FUNDI WA MPIRA SHAABAN KIPRESHA, AJIKITA KWENYE UKOCHA MDAULA

Na Ayubu Mhina. Pwani

Kwa wakazi wa Mdaula kata ya Bwilingu, Chalinze wilayani Bagamoyo wanamfahamu vema kwa jina la Shaaban Hussein Kipresha akiwa kama mkufunzi wa Mdaula United.

Kipresha amewahi kulisakata kabumbu la ushindani jijini Dar es Salaam, mwenyewe anasimulia kuwa amewahi kukipiga Jah People ya Magomeni Mikumi mtaa wa Ifunda, Baghdad pia ya Makuti mtaa wa Shoka sambamba na Big Bonn ya mtaa huo huo, anadai akiwa Big Bonn amecheza na wakali kama Habib Mahadhi, Khalid Ngome, Gidion Kaburi, Dyson Abiola na wengineo lakini alipokuwa Baghdad alicheza na Godfrey Kalumbeta, Hamza Mtaalamu na Jah People amecheza na George Kavila.

Kipresha alikuwa akicheza namba nane yaani kiungo, anawakumbuka sana akina Athuman Machupa, Jabir Aziz "Stima", Shekhan Rashid na wengineo ambao anakiri aliwafunika vilivyo lakini bahati haikuwa yake na akajikuta anaangukia mtaani na sasa ni kocha wa Mdaula United ya Mdaula inayoshiriki Ligi Daraja la tatu Pwani.

Kipresha tayari amehitimu kozi ya awali ya ukocha (Priliminaly Course) mjini Morogoro na sasa ni kocha mwenye uwezo wa kukaa benchini kuziongoza timu za madaraja ya chini kama hiyo ya Mdaula United na amedai lengo lake ni kusomea zaidi ukocha ili akazinoe timu za Ligi Kuu Bara, mwenyewe anadai anataka awe kama Fred Minziro kwa ngekewa ya kuzipandisha timu Ligi Kuu na yeye anataka kuanza na Mdaula United ambapo ameapa kuipandisha daraja la pili

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa