Tenga, Mwenyekiti mpya BMT

Na Saida Salum. Dar es Salaam

Waziri wa Habari, Michezo, Sanaa na Utamaduni, Mhe Harrison Mwakyembe amemteua Leodegar Chila Tenga kuwa mwenyekiti mpya wa Baraza la Michezo la Taifa, (BMT) akimrithi Dioniz Malinzi aliyefutwa kazi.

Tenga amewahi kuhudumu kama Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini, (TFF) ataanza majukumu hayo kuanzia sasa na pia ana kazi kubwa kuhakikisha michezo nchini inapiga hatua.

Nahodha huyo wa zamani wa timu ya taifa, Taifa Stars iliyobahatika kufuzu kwa mara ya kwanza fainali za mataifa Afrika zilizofanyika Lagos Nigeria mwaka 1980, pia amewahi kuzichezea Yanga Sc na Pan Africans

Leodegar Tenga mwenyekiti mpya wa BMT

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI