Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Stand United yaizamisha Singida United

Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam

Timu ya Stand United ya mkoani Shinyanga, jana imeifunga Singida United bao 1-0 mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uwanja wa Namfua mkoani Singida.

Huo ni mwendelezo mzuri kwa Stand United ambao wameanza kujiondoa taratibu katika janga la kushuka daraja lakini pia yamekuwa matokeo mabaya kwa Singida United inayonolewa na Mholanzi Hans Van der Pluijm katika vita ya kuwania ubingwa wa bara.

Endapo Singida United ingeibuka na ushindi katika mchezo huo ingepaa hadi nafasi ya pili kwakufikisha pointi 36, sasa inabaki katika nafasi yake ya nne ikiwa na pointi 33 wakati Stand iliyokuwa nafasi ya 12 na pointi zake 16 sasa inakwea hadi nafasi ya 8 ikiwa na pointi 19 sawa na Mbao Fc ambao nao wametoka sare tasa 0-0 na Mtibwa Sugar uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Matokeo mengine, Njombe Mji Fc ililazimishwa sare tasa na Mbeya City uwanja wa Sabasaba Njombe, na kikosi cha Ruvu Shooting kikaikandika Lipuli Fc ya Iringa mabao 3-1 uwanja wa Mabatini, Mlandizi Pwani, leo hii Kagera Sugar wanaikaribisha Azam Fc uwanja wa Kaitaba, Bukoba

Kwa habari kamili gonga www.mambouwanjani.

Stand United wakishangilia ushindi 

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa