Ruvu Shooting yaiweka "Danger Zone" Kagera Sugar

Na Ikram Khamees. Dar es Salaam

Timu ya Ruvu Shooting ya Mlandizi mkoani Pwani, jana jioni imeichapa Kagera Sugar mabao 2-0 mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara katika uwanja wa Mabatini, Mlandizi Kibaha Pwani.

Ushindi huo unaifanya Ruvu Shooting inayonolewa na Abdulmatik Haji kufikisha pointi 17 na kuchupa hadi nafasi ya 12 katika msimamo wa Ligi Kuu Bara huku sasa ikiiweka shakani Kagera Sugar ikichungulia tundu la kushuka daraja.

Mabao ya Ruvu Shooting yenye msemaji wake asiyeishiwa maneno, Masau Bwire yalifungwa na Khamis Mcha "Vialii" dakika ya 55 na Alinanuswe Martin dakika ya 79

Ruvu Shooting imeifunga Kagera Sugar

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI